.

.

.

KUJIUNGA NA PAGE YETU YA FB NA TWITTER BONYEZA HAPA >FACEBOOK<>TWITTER<

KILELE CHA UBEPARI TANZANIA NA AFRIKA


KILELE CHA UBEPARI TANZANIA NA AFRIKA

Afrika imefika hapa ilipofika sasa kwa sababu wazee wetu waliviona hivi viashiria vya ubepari toka mwanzo lakini hawakuchukuwa hatua za msingi kuvidhibiti zaidi ya wengi wa wazee wetu walizidi kukuza fadhila za walowezi wakiamini ndio mwazo wa maendeleo katika nchi zetu.Elimu ya kugundua kuwa hivi ni viashiria vya ubepari katika afrika na vina madhara gani kwa usitawi wa bara letu ilikuwa bado ndogo ndani ya viongozi wetu na wananchi kwa ujumla.
Shukurani za dhati kwa HAYATI MWALIMU  JULIUS  KAMBARAGE  NYERERE kwa kuona hili mapema na kugundua kuwa makabila na dini ni zao la ubepari hivyo basi akaunda serikali isiyoegemea kwenye kabila lolote au dini yoyote ile. Akasimamia umoja wa kitaifa ingawa ilikuwa ngumu sana maana machifu na wakuu wa koo walikuwa wameshalewa na ubepari huu mdogo ndani ya roho zao.
Mwalimu akishirikiana na waasisi wengine wa taifa wakatengeneza azimio la Arusha lengo lilikuwa moja tu kujaribu na kuhakikisha huu ubepari mdogo unaisha ndani ya nchi.Wakasimamia kwa nguvu zao zote lakini kazi ikawa bado ngumu.
Azimo la Arusha liliposhinda kufanikiwa nchini ilikuwa ni sherehe tosha kwa mabepari wa dunia hii maana lingeleta kikwazo kikubwa kwao katika utekelezaji wa shughuli zao za kila siku nchini kama wananchi wote wangelikubali kwa roho moja.
Hili ndilo lilikuwa pigo kubwa kwa masikini wote wa taifa hili, pindi mkombozi wetu(azimio la Arusha) alipofariki baada ya kushindwa nguvu na mabepari neema yetu,asali yetu,saruji yetu,chakula chetu,na kila kitu chetu kilikufa nae.
Azimio liliondoka na faraja ya masikini  Tanzania, faraja ya masikini afrika ,faraja ya masikini wa dunia.Mizani ya usawa ikavunjika vipande vipande kutokana nakuelemewa na mzigo wa upande mmoja.
Mimi alipata nguvu kubwa kuliko sisi.wachache wakawa wakuu wa maamuzi kuliko wengi, wazawa wakawa wageni barani afrika na wageni wakawa wazawa.huu ndo ufalume wa ubepari ulipo fanikiwa na kutupa walo wengi chini hi indo maana ya kura ya VETO.
Mtu mmoja ana uwezo wa kutumia kura yake kupinga kura za taifa zima au jumuiya zima hivyo wangonge wanakuwa hawana tena dhamani mbele ya wachache wanaoweza kupiga kura juu ya mstakabali wa maisha yao ya sasa na baadae.




Elimu inamchango mkubwa wa waziwazi wakuuwa usawa(ujamaa) katika nchi nyingi za afrika.Tukiangalia elimu ya kikoloni ilimjenga mtu kuwa tofauti na wengine kuwa na aina tofauti ya jamii alipotokea.mbinu nyingi za uzalishaji na utunzaji kumbukumbu kitu ambacho kiliwafanya wengi wazitumie mbinu hizo vibaya kwa kuiba na kudhulumu kirahisi.
Elimu ilimfanya mtu kujisikia, kupenda anasa na maisha ya kifahari kitu ambacho kilichangia kwa kiasi kikubwa kuuwa ujamaa uliokuwa nchini.tukumbuke kuwa Mwalimu Julius kambarage Nyerere alijitahidi kwa kiasi kikubwa kuondoa hali hii ndani ya nchi yetu lakini alishindwa kutokana kukosa ushirikiano ndani ya wasomi wa nchi hii walikuwa wanataka kazi nzuri nyumba zuri na maisha ya kifahari kuliko hata hali halisi ya taifa letu.
Mila na desturi zetu zilizowafanya machifu kuwa na mali nyingi na wake wengi kwa kiasi Fulani zilipunguza mvuto wa ujamaa na kujitegemea maana chifu alikuwa na wingi wa mali kuzidi jamii iliyomzunguka hali hii kwa kiasi Fulani ilileta chuki ndani ya jamii.
Sababu nyingine nyingi kama ongezeko la watu, ugumu wa ufatiliaji,ukubwa wa nchi,na majanga ya kitaifa kama vile njaa viliweza kupunguza kasi ya azimio la Arusha kwa kiasi fulani.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...