Safari za
wafanyabiashara ziliwezesha kugundulika kwa bara hili la kwa mataifa ya magharibi na asia kwa
ujumla wake.Bara letu lilionekana kuwa eno la wazi lisilo na miliki wenye nguvu
kwa kuwa kulikuwa na makabila waliokuwa wamejitenga sana kiumbali na huku
yakijishuhulisha nza shuhuli mbalimbali ikiwemo uvuvi,ufugaji na mengine kilimo
basi nchi za bara la ulaya waliamua kwa dhati kushambulia bara hili kila kona
na kujichumia mali zilizopo na pia walichukuwa watu wa bara hili na kwenda
kuwafanyisha kazi ngumu kwenye mashamba na viwandani. Hakuna kilichokuwa si
mali kwao, vyote walibeba si pembe za ndovu,watu ,madini wala bidhaa za
utamaduni.Ingawa maeneo mengine walipata vizuizi kutoka kwa makabila kadhaa yaliokuwa na vifaa
vya kivita na kundi kubwa la wapiganaji lakini kwao haikuwa shida kubwa maana
walikuwa wamesha jipanga sawa sawa kuvunja kizuizi chochote kile kitachokuwa
kinajitokeza na kuzuia mpango yao.huku wakitengeneza ramani ya kuonyesha sehemu
zenye mali ikiwemo madini na maeneo yanayofaa kwa kilimo walifanya kazii hii
kwa uangalifu mkubwa.