Tutambue kuwa ubepari
huanza kwa hatua hiyo basi historia inaonyesha kuwa toka aumbwe Adamu na Eva
hapo ndipo ubepari ulipoaza ukiwa na sura ya ubinafsi(maana ubinafsi ni mtoto
wa ubepari).Adamu na Eva walipewa dunia waitawale na wafaidi kila kitu
kilichopo ndani ya dunia hii mto,maziwa ,asali ,matunda, majani na kadhalika.
Adamu na Eva alijua
kabisa bosi wao ni Mungu aliye juu mmiliki wa mali zote walizokabiziwa wazitumie
mpaka pumzi yao pia ilikuwa ni mali yake.
Adamu na Eva walingizwa kishawishini na shetani wamsaliti
Mungu na kubinafsisha mali zake zote walizokabiziwa na wazimiliki wao kwa
ushirikiano na shetani mkuu wa kuzinu.
Kutokana na hilo bwana
Mungu alichukiza na ile hali na kuamua kuwatupa nje ya ile bustani ya edeni na
kuwaacha wakahajitafutie wenyewe chakula na mahitaji yao ya kila siku.
Katika hali hii basi
tutaona kuwa mwenyekiti wa ubepari duniani ni SHETANI.
Maana ndiye muanzilishi
waubepari duniani toka enzi za Adamu na Eva ni yeye aliyewapa ujasiri wakina
Adamu na Eva waukubali ubinafsi na kuachana na mpango wa Mungu ulikuwa unaweka
umoja wa kila kitu.