.

.

.

KUJIUNGA NA PAGE YETU YA FB NA TWITTER BONYEZA HAPA >FACEBOOK<>TWITTER<

UTANGULIZI


Tujikumbushe kwanza Africa ilitoka wapi ?Africa kama mabara mengine dunia  lilikuwa bara lenye wananchi wanaojiongoza kwa  mila na desturi za makabila yao.Hii ikimaanisha kuwa sheria na taaratibu za kuishi zilizingatia sana mila na desturi hiyo basi kila ukoo ulifanya kila mbinu ili uweze kukubalika katika kabila husika na waweze kupewa uongozi wa kabila husika,hali hii ilifanya kupatikana kwa ukoo zenye nguvu ya kutawala na kutoa maamuzi mazito kuhusu makabila husika.
 Katika hali hii iliongeza ubunifu hasa katika maeneo ya uzalishaji wa mazao na vifaa vya kivita na mafunzo ya kijeshi.hii ilisaidia sana ukuwaji wa maeneo na kusababisha koo na makabila mengine madogo madogo kufa kwa sababu ya kushindwa  kivita na mali zao walizokuwa wakimiliki kupokonywa na makabila hayo yakageuka vibaraka wa makabila yale makubwa.
Makabila mengi yalipotea nakutofahamika tena kwenye uso wa dunia kutokana na sababu hizo na mengine yaliweka makazi kwenye maeneo yenye wanyama wakali ,mafuriko na wadudu waambukizao maradhi  na wakashambuliwa na magonjwa,wanyama wakali na mafuriko  na kuisha taratibu baada ya kuanza kutawanyika kukimbia majanga hayo.


 


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...